Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama
Updated at 21 Sep 2017 10:05
Edited By, Melkisedeck Shine, at 2017.
Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama
Mahitaji
Ndizi mbichi 6
Nyama ya ng'ombe (nusu kilo)
Viazi mviringo 2
Kitunguu swaum
Tangawizi
Kitunguu maji
Nyanya 1 kubwa
Mafuta (vegetable oil)
Chumvi
Limao
Pilipili
Matayarisho
Chemsha nyama na limao, kitunguu swaum, tangawizi chumvi na maji kiasi mpaka nyama iive, Hakikisha unaiacha na supu kiasi kwa ajili ya kuwekea kwenye ndizi.Kisha katakata nyanya na vitunguu na uweke pembeni .Menya ndizi na viazi kisha zichemshe pamoja na vitunguu, nyanya, maji kidogo, mafuta na uhakikishe haziivi kabisa. Baada ya hapo tia nyama na supu yake, pilipili mzima na chumvi na uache uchemke mpaka ndizi na viazi viive.Na baada ya hapo mchemsho wako utakuwa tayari kwa kuliwa
[MUHIMU HII] Msimu huu usipitwe na dawa hii muhimu ya kuandalia shamba
Soma na kutoa Maoni kuhusu Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama
Endelea kusoma makala hizi zinazofanana na hii ya, Mapishi ya Mchemsho wa ndizi na nyama;
.
Post preview:
Close preview